Machapisho

Chid Benz Arudi Mtaani Baada ya Miezi 10 ya Marekebisho

Picha
Msanii maarufu wa muziki wa Hip Hop nchini Tanzania, Chid Benz, amerudi mtaani baada ya kukaa kwa takribani miezi 10 kwenye nyumba ya marekebisho akipatiwa matibabu dhidi ya uraibu wa dawa za kulevya. Chid Benz, ambaye kwa muda mrefu alikumbwa na changamoto ya matumizi ya dawa za kulevya, amesema sasa yuko tayari kuanza ukurasa mpya wa maisha yake na amejipanga kulitumikia taifa kupitia kipaji chake cha muziki pamoja na kushirikiana na jamii katika mapambano dhidi ya dawa hizo. > "Nashukuru Mungu kwa kuniweka hai na kunipa nafasi ya pili. Nipo tayari kuonesha mfano bora na kusaidia vijana wenzangu kuepuka makosa niliyopitia," alisema Chid Benz. Mashabiki wake wengi wamepokea kwa furaha taarifa za kurejea kwake, wakimtakia kila la heri katika safari yake mpya ya maisha na sanaa. Wengi wanaamini kurejea kwa Chid Benz kutarudisha ladha ya Hip Hop ya Tanzania ambayo kwa muda imekuwa ikikosa sauti yake ya kipekee. "Habari hii imeletwa kwako na Habari 255"🇹🇿

Puma yaibuka msambazaji mpya wa mipira EPL baada ya miaka 25 ya Nike

Picha
Kampuni ya vifaa vya michezo Puma ndiyo wasambazaji wapya wa mipira inayotumika kwenye Ligi Kuu England (EPL) kuanzia msimu huu, ikibadilisha rasmi nafasi iliyoshikiliwa na Nike kwa zaidi ya miaka 25. Uamuzi huu umeleta upepo mpya katika ligi maarufu zaidi duniani, huku mpira mpya wa Puma ukitajwa kuwa na teknolojia ya kisasa inayoongeza kasi na mabadiliko ya ghafla hewani – jambo ambalo tayari limeanza kuonekana kama changamoto kubwa kwa makipa. Kwa mujibu wa ripoti kutoka England, mpira huo mpya unaundwa kwa mfumo maalumu unaosaidia urahisi wa kupiga kwa usahihi na kuongeza nguvu za shuti. Wachezaji wengi wameonekana kufurahia, lakini upande wa makipa, mpira huo umeelezwa kuwa “tishio” kutokana na mabadiliko yake ya ghafla angani na kasi kubwa ya kuelekea langoni. Hii ni mara ya kwanza tangu msimu wa 2000/01 ambapo ligi hiyo inatumia mpira usio wa Nike, hatua ambayo pia inatarajiwa kuimarisha ushindani wa kibiashara katika soko la vifaa vya michezo duniani. Mashabiki wengi wanataraji...

Tume ya Uchaguzi na NIDA Zakanusha Madai ya Humphrey Polepole

Picha
Dar es Salaam – Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)  zimekanusha madai yaliyotolewa na aliyekuwa Mbunge wa CCM, Humphrey Polepole, kuwa mifumo ya taasisi hizo imeunganishwa na chama tawala CCM. Katika taarifa zao kwa vyombo vya habari, taasisi hizo zimesisitiza kuwa hazina uhusiano wa moja kwa moja na chama chochote cha siasa na kwamba mifumo yao inafanya kazi kwa uhuru na kwa mujibu wa sheria za nchi. Msemaji wa NEC alieleza: > “Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni taasisi huru kikatiba. Hatujawahi, hatuna, wala hatutakuwa na mfumo wowote ulio na muunganiko na chama cha siasa. Kazi yetu ni kusimamia chaguzi kwa uwazi na kwa mujibu wa Katiba.” Kwa upande wake, NIDA imeeleza kuwa jukumu lake kuu ni kusajili na kutoa vitambulisho vya taifa kwa Watanzania, na si kushirikiana na vyama vya siasa. > “Hakuna mfumo wa NIDA unaohusiana na chama chochote. Mfumo wetu ni wa kitaifa na unahusiana tu na huduma za umma,” ilisomeka sehemu ya taarifa ya NIDA. M...

Simba SC Yamnyakua Neo Maema Kutoka Sundowns |

Picha
  Klabu ya Simba SC imefanikiwa kukamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji kutoka Afrika Kusini, Neo Maema, akitokea Mamelodi Sundowns. Usajili huu unatajwa kuwa moja ya hatua kubwa za maandalizi ya wekundu wa Msimbazi kuelekea msimu mpya wa Ligi Kuu Bara na michuano ya kimataifa ya CAF Champions League. Neo Maema, mwenye sifa ya kucheza nafasi nyingi za kiungo cha ushambuliaji, amekuwa akiwika katika Ligi Kuu ya Afrika Kusini (PSL) kutokana na kasi yake, pasi zenye ubunifu na uwezo wa kupiga mashuti ya mbali. Katika kikosi cha Sundowns, alikuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya klabu hiyo, lakini ushindani mkubwa wa namba ulimfanya kufikiria changamoto mpya. Akizungumza mara baada ya kuwasili Dar es Salaam, Maema alisema: > “Najivunia kujiunga na Simba SC, klabu kubwa yenye historia na mashabiki wengi barani Afrika. Nipo tayari kutoa mchango wangu kuhakikisha timu inafanikisha malengo yake.” Uongozi wa Simba SC umethibitisha kuwa usajili wa Neo Maema ni sehemu ya mikakati ya kuonge...

Vyakula aina nane ambavyo vitakufanya utoe hewa chafu

Picha
Kutoa hewa chafu ni kawaida, mtu wa kawaida hufanya mara 5-15 kwa siku. Kwa kweli, kuwa na gesi nyingi kwa siku fulani inaweza kweli kuwa ishara ya afya njema, ikiwa unasahau kuhusu usumbufu wowote au aibu iliyoweza kusababisha. Hiyo ni kwa sababu vyakula vinavyotengeneza hewa chafu huwa na wanga, zenye nyuzinyuzi nyingi, ambazo mwili wako hauwezi kuzivunjavunja lakini bakteria kwenye utumbo wako wanaweza. Kwa hivyo ni vyakula gani vinakufanya utoe hewa chafu, ambayo hewa yako yako kuwa na harufu, na unapaswa kushauriana na daktari wakati gani? 1. Vyakula vya mafuta Vyakula vya mafuta hupunguza kasi ya usagaji chakula, jambo ambalo linaweza kuviacha vikiwa kujazana kwenye utumbo wako, vikichacha na kutoa harufu mbaya. Nyama za mafuta ni ngumu kwa sababu zina wingi wa amino acid methionine, ambayo ina sulphur.  Sulphur huvunjwa na bakteria wa utumbo wako kuwa salfa ya hidrojeni, harufu ya yai lililooza na 'huongeza' harufu ya gesi inayotolewa na vyakula vingine unavyokula pamoj...

Trump: Kwa kuishambulia Iran, tulizuia 'vita' Mashariki ya Kati

Picha
Rais wa Marekani Donald Trump anasema iwapo Iran itarejelea mpango wake wa kurutubisha nyuklia, itashambuliwa tena na Marekani. Bw.Trump, akijibu maswali ya wanahabari katika Ikulu ya White House siku ya Jumatano, alisisitiza kwamba Marekani imezuia vita katika eneo la Mashariki ya Kati kwa kuizuia Iran kupata silaha za nyuklia. Kulingana na Bw. Trump, kabla ya Marekani kushambulia vituo vya nyuklia vya Iran vilivyo chini ya ardhi, nchi hiyo ilikuwa "miezi miwili tu kabla ya kupata silaha ya nyuklia." "Tuliondoa uwezo wao wa kutengeneza silaha za nyuklia," Bw. Trump alisema, akiwa ameshikilia kielelezo cha bomu la B-52. "Iran ingeweza kuwa na silaha ya nyuklia ndani ya miezi miwili au chini ya hapo, lakini iliharibiwa kabisa." "Tulizuia vita katika Mashariki ya Kati kwa kuzuia Iran kupata silaha ya nyuklia," Bw. Trump alisema. "Wanaweza kusema wataanza tena, lakini hiyo ni hatari kwao kwa sababu tutarudi." Kulingana na Bw. Trump, "...

Siwezi Acha kuzungumza kama watu wanatekwa....Gwajima

Picha
Maelezo ya picha, Mbunge wa Kawe, Dar es Salaam Tanzania kupitia CCM na Askofu Josephat Gwajima Mbunge wa Kawe, mkoa wa Dar es Salaam Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Askofu wa Kanisa la Glory Of Christ Tanzania, Josephat Gwajima amesema hawezi kuacha kuzungumza kama watu wanatekwa. Gwajima ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari, kufuatia miezi kadhaa ya mvutano na chama chake cha Siasa tangu akemee matukio hayo mwezi Mei mwaka huu. “Kuhusu utekaji siogopi mtu, hata kama makanisa yatafungwa kwa miaka 100, siwezi kuacha kuzungumza kama watu wanaendelea kutekwa. Hakuna kutekana, hakuna kuumizana. Sijasema CCM inateka, lakini ndiyo chama kilicho madarakani.” Ameeleza njia pekee ya kukomesha vitendo hivyo ni kutoa ulinzi kwa wakuu wa vyombo vya usalama ili wasipate matatizo kutoka kwa wakuu wao wa kisiasa pale wanapolinda nchi. Pia ametaka vyombo vya dola viwekwe mbali na siasa. Gwajima ameweka wazi kwamba ataihama CCM, na kuongeza kwamba bado ni mwanacha...